Sunday, August 20, 2017

KILIMO BORA CHA BILINGANYA NA KANGETAKILIMO




                                                                                                                                               




EMMANUEL KANGETA
Tell:+255717274387
Whatsapp: +255717274387
Email:emmanuelkangeta@gmail.com or
Email:kangetakilimo@gmail.com
Web: kangetakilimo
Twitter: 
kangetakilimo                                                                                                                                              
Fb: kangetakilimo or emmanuelkangeta








KILIMO CHA BILINGANYA

Zao hili asili yake ni sehemu za nchi ya India nchi inayo ongoza dunia kwa kilimo cha Bilinganya ni uchina hasa katika pwani za kusini mwa china inayo lima asilima 59% duniani ikifuatiwa na India Uturuki,Misri Irani na Italy.`Bilinganya imo katika jamii ya mimea inayohusisha nyanya, pilipili, viazi mviringo na nyanya mshumaa. Mboga hii ina viinilishe muhimu kama vile madini aina ya chokaa na chuma, vitamini A, B hadi C, wanga, protni na maji. Mboga hii hutumika kutengeneza supu au kama kiungo katika vyakula mbalimbali. Vile vite huweza kuhifadhiwa kwa kukatakata vipande na kuwekwa kwenye makopo. Zao hili huhitaji hali yajoto la wastani, udongo wenye kina kirefu na rutuba ya kutosha na usiotuamisha maji. Kwa kawaida bilinganya hulimwa zaidi ya msimu mmoja, lakini katika nchi za Kitropild (joto) zao hili hulimwa kwa msimu mmoja. Zao hili huhitaji haliyahewa ya joto hu

weza pia kulimwa si chini ya nyuzi 10 oc lakini hustawi vizuri katika nyuzi 26 oc hadi 30 oc

AINA ZA BILINGANYA:
Kuna Aina za bilinganya zinazolimwa kwa wingi katika nchi za ukanda wajoto ni kama zifuatazo:-
ü  Black Beauty:
Aina hii huzaa sana, matunda yake meusi, makubwa, na ya mviringo.



Aina ya Bilinganya Black Beauty
ü  Florida Market
Matunda ya Florida Market yana umbo Kama yai. Aina hii pia huzaa sana, lakini hushambuliwa kwa urahisi na ugonjwa wa mnyauko bakiteria (Bacterial wilt).

ü  Florida High Bush
Matunda yake ni makubwa ycnye umbo la yai na rangi ya kijani kibichi iliyochanganyika na nyeusi.

ü  NewyorkSpineless
Matunda ya Newyork Spineless ni ya mviringo, makubwa na yana rangi ya zambar

au.
-

ü  Peredeniya
Aina hii huzaa sana, matunda yake ni makubwa kiasi na yana umbo la yai.


Aina zingine za bilinganya ni
Matale, Kopek na Rosita.
Aina hizi huvumilia sana mashambulizi ya ugonjwa wa mnyauko bakteriaf

JINSI YA KUANDAA KITALU
 Kitalu ni sehemu maalumu iliyopangiliwa kwa ajili ya kutunzia miche michanga kabla ya kuipeleka shambani ama bustanini. Sio mimea yote inahitaji vitalu ila mimea mingi inahitaji vitalu. Mimea Kama bilinganya.Mimea ambayo inachelewa kuchipua, kukua, na yenye kuhitaji matunzo au kuhudumiwa kwa karibu wakati ikiwa michanga inashauriwa ipandwe kwanza kwenye kitalu hadi itakapopata miche inayotakiwa kisha kupandikizwa bustanini au shambani. Weka udongo debe mbili, mbolea debe moja na makapi ya mpunga ama mchanga debe moja (2:1:1). Changanya vizuri kwa kutumia koleo na utandaze huo mchanganyiko kwa kutumiaa reki. Panda au sia mbegu bora ambazo zimekomaa na kukauka vizuri, ambazo hazijashambuliwa na magonjwa au wadudu na zenye uwezo wa kuota vizuri zikipandwa. Kama unahitaji kununua mbegu inashauriwa kununua

mbegu kutoka kwa mawakala wanaoaminika. Unaweza kupanda kwa mstari ama kwa kusia. Miche ikiwa tayari ikapandwe bustanini wakati wa jioni na imwagiliwe vizuri. Bustani iwe imeandaliwa kabla ya siku ya kuhamisha miche. Gramu 500 za mbegu zinatosha kupandikiza katika eneo la hekta moja. Nafasi kati ya mstari na mstari iwe sentimeta 10 hadi 15 na kina kiwe sentimita 1.5. Baada ya kusia mbegu fukia na tandaza nyasi kavu na kisha mwagilia maji. Endelea kumwagilia kitalu kila siku, asubuhi na jioni, hadi mbegu zitakapoota. Mbegu huota baada ya siku ya 10 hadi 12.Udongo kwenye kitalu unatakiwa uwe unaweza kupitisha maji vizuri. Tayarisha kitalu chako kwa kuchimba au kulima udongo angalau 30 sm kwenda chini, ondoa mabaki yoyote ya mimea na mizizi na vunja mabonge yote ya udongo kisha changanya samadi iliyooza vizuri au mboji iliyoiva vizuri. Sawazisha vizuri na reki hadi udongo uwe vizuri.
Pima upana na urefu wa kitalu ambao utakuwezesha kufikia kila pembe ya kitalu kwa urahisi bila kukanyaga ndani ya kitalu. Hii itasaidia kupunguza uwezekano wa kuleta magonjwa kwenye kitalu na itarahisisha kungoa magugu pamoja na kuhamisha miche kwenda shambani.
Kama unasia mbegu katika mistari hakikisha kuwa mistari ipo katika umbali  Baada ya kusia mbegu funikia na udongo kidogo kutegemea na ukubwa wa mbegu. Siku moja kabla ya kusia mbegu, mwagia kitalu maji hadi kilowe vizuri. Kwa siku zinazofuata inashauriwa kumwagilia maji kidogo kidogo hadi pale zitaka

 Sifa za sehemu nzuri ya kutengeneza kitalu
 Karibu na chanzo cha maji au bomba.
 Sio mbali na shambani/bustanini.
 Mbali na wanyama ama kuwe na uzio.
 Pasiwe na upepo mkali
 Iwe na kivuli.
 Iwe karibu na njia kurahisisha usafirishaji pindi ikibidi.

Matunzo ya kitalu
Baada ya kusia mbegu hakikisha kitalu hakipati jua la moja kwa moja na mvua kubwa. Weka matandazo ya majani ili kusaidia udongo kuhifadhi unyevunyevu na kuweza kuzuia mwangaza wa jua wa moja kwa moja.
Angalizo:
 Ondoa matandazo mara tu mbegu zitakapochipua
 Ruhusu kivuli kidogo kwenye miche na usiweke kivuli kikubwa sana kwani kitaifaya miche isikue
 Baada ya kuchipua mwagilia maji taratibu kwa kutumia bomba au chupa yenye vitundu vidogo dogo. Hakikisha maji hayazidi kwenye kitalu kwani yanaweza kusababisha ugonjwa na miche kuharibika.
 Hakikisha kitalu ni kisafi wakati wote. Ondoa magugu yoyote yatakayojitokeza.
 Punguzia miche kama imejazana sana ili kuipa nafasi ya kukua vizuri.
 Kagua kitalu mara kwa mara kuangalia kama kuna uvamizi wowote wa wadudu waharibifu au mlipuko wa ugonjwa.

Baada ya miche yako kufikia muda wa kupandikiza inashauriwa kuchagua miche yenye afya nzuri ambayo haijaathirika na wadudu wala kuwa na dalili yoyote ya ugonjwa.
Mwagilia maji kwenye kitalu usiku mmoja kabla ya siku ya kung’oa ili kurahisiha ung’oaji na kuzuia uwezekano wa mizizi kuharibika. Hakikisha miche iliyong’olewa haipati jua la moja kwa moja au hewa yenye joto. Inashauriwa kuiweka kwenye trei au kikapu na kuifunika na majani au nguo mbichi wakati inapelekwa shambani au bustanini.
Namna ya kupandikiza miche kwenye Shambani/Bustanini
 Panga kupandikiza miche shambani au bustanini siku ambayo jua siyo kali sana au wakati wa jioni wakati jua linakaribia kuzama.
 Manyunyu ya mvua ni muhimu na husaidia sana wakati wa kupandikiza.
 Shindilia udongo vizuri kuzunguka mizizi ya mche kwa kutumia vidole vyako ili kuufanya mche ujishike vizuri kwenye udongo.
 Hakikisha unaweka nafasi ya kutosha kati ya mmea na mmea na mstari hadi mstari ili kuacha nafasi ya mizizi kutanukia na majani kuchanulia hapo baadaye.
 Kama hamna mvua wakati wa kupandikiza inashauriwa kumwagilia hata kama mimea haionyeshi dalili za kukauka.
 Ikinge mimea iliyopandikizwa na jua la moja kwa moja hadi wakati ambapo itaonyesha kuwa imeshika kwenye udongo, inaweza kukua yenyewe na kuhimili mwanga wa jua.

Faida za Kitalu cha miche kwa mkulima
 Kuchagua miche iliyo na afya nzuri.
 Kuthibiti magugu shambani kabla hajahamishia miche shambani.
 Kupata miche ya kupanda muda wowote atakao.
 Ni rahisi kuthibiti vijidudu viharibifu na magonjwa kwenye kitalu kuliko shambani ama bustanini. Hii ni kwa sababu kitalu kinakua na miche mingi na

KUHAMISHA MICHE YA BILINGANYA KATIKA KITALU
Miche huwa tayari kwa kupandikizwa shambani baada ya wiki sita hadi nane. Wakati huu huwa na urefu wa sentimita 15 mpaka 20 (sawa na urefu wa kalamu ya risasi).
Mwezi mmoja kabla kupanda miche, rutubisha udongo kwa kuweka mbolea za asili zilizooza vizuri. Mbolea hizi ni kama samadi, mbolea vunde na mbolea ya kuku.
Weka kiasi cha tani 10 hadi 20 kwa hekta. Kiasi hiki ni sawa na kuweka ndoo moja hadi mbili zenye ujazo wa lita 20 katika eneo la mita mraba moja. Mbolea ya mchanganyiko aina ya N.P.K yenye uwiano wa 20:10:10 huwekwa kwenye shimo wakati wa kupandikiza mche. Kiasi kinachohitajika ni gramu tatu hadi tano (sawa na nusu kijiko mpaka kijiko kimoja kidogo cha chai) kwa kila shimo.
Nafasi ya kupandikiza hutegemea aina ya bilinganya. Aina ndogo hupandikizwa katika nafasi ya sentimita 80 mpaka 100 kutoka mstari hadi mstari na sentimita 50 mpaka 60 kutoka mche hadi mche. Aina kubwa hupandikizwa katika nafasi nafasi ya sentimita 80 mpaka 100 kutoka mstari hadi mstari na sentimita 80 mpaka 90 kutoka mche hadi mche. Kazi ya kuhamisha miche ifanyike kwa uangalifu mkubwa ili kuepuka kuikata mizizi.
Hali ya Udongo
Huhitaji udongo wenye rutuba nzuri ulio na virutubisho. Vile vile haihitaji udongo wenye kiasi kikubwa cha tindikali na alikali kubwa. Hali ya udongo katika
kipimo cha pH kiwe kati ya 6.0 na 7.0. Ingawa mmea una uwezo vile vile wa kuhimili kwenye udongo wenye pH 5.0
AINA ZA UDONGO
Kuna aina kuu tatu za udongo,
• Kichanga (Sand soil) –
una uwezo mdogo wa kuhifadhi maji na unyevunyevu. Hivyo, hukauka upesi.
• Tifutifu (Loam soil) –
 unahifadhi maji vizuri na upatikanaji wa maji na virutubisho kwa mimea ni mkubwa.
Mfinyanzi (Clay soil) –
 unahifadhi maji mengi zaidi, bali upatikanaji wa virutubisho kwa mimea ni mdogo.

Vipimo vinavyoonyesha hali ya rotuba ya udongo ni:
• Tindikali ya udongo
• Kiasi cha mboji
• Kiasi cha Naitrojeni, Fosfati, Potashi, Salfa, Chokaa (Calcium) na Magnesium. Vilevile kiasi cha zinki, shaba, manganese na boroni vinapimwa.

Kipimo cha PH ya udongo (Soil pH)
PH ni kipimo kinachoonyesha kiwango cha tindikali au nyongo katika udongo. Udongo waweza kuwa na tindikali (ph ndogo kuliko 7), nyongo (ph kubwa kuliko 7), au katikati (neutral) - ph ya 7.Tindikali au nyongo ya udongo hupimwa kwa kutumia pH mita. Mazao mengi hustawi zaidi katika udongo wenye hali ya tindikali ya wastani (kipimo cha pH 5.5 hadi 7.0).

 bilinganya hustawi katika udongo wowote ambao hautuamishi maji.Hivyo zao hili linaweza kulimwa katika maeneo yoyote na pia linaweza kulimwa katika udongo wenye asili ya mfinyanzi katika maeneo yanayopata mvua kwa kiasi kidogo.

Matandazo (Mulches)
Matandazo ina maana ya kutumia nyasi na mabaki ya mimea mingne kufunika aridhi. Baada ya miche kutambaaa kwa kiasi unaweza kuweka matandazo (mulches) ambayo yaweza kuwa nyasi kavu kwenye udongo ili kuzuia upotevu wa unyevu vile viile kupunguza uotaji wa magugu shambani kwako. Vile vile matandazo yakioza yanaongeza rutuba kwenye udongo na hulinda udongo dhidi ya mmomonyoko wa udongo.

Palizi
Hakikisha shamba ni safi wakati wote ili kuzuia ushindani wa chakula, maji na mwanga kati ya mimea na magugu. Usafi wa shamba pia huondoa maficho ya wadudu waharibifu na huzuia kuenea kwa magonjwa

MBOLEA
Mbolea ni chakula cha mimea, ambayo ni mchanganyiko wa virutubisho mbalimbali vinavyoongezwa kwenye udongo au vinavyowekwa moja kwa moja kwenye mimea ili kuongeza ukuaji na uzalishaji wa mimea.
Virutubisho hivyo ni pamoja na madini muhimu kama vile naitrojeni, fosfati na potashi. Madini mengine ni pamoja na salfa, chokaa (calcium), magnesium, boroni, shaba, chuma, manganese, molybedenum na zinki. Haya madini kwa asili, yanapatikana katika udongo kwa viwango tofauti. Yanapopungua kutokana na kilimo, inabidi yaongezwe kwa kutia mbolea.

Aina za mbolea
Kuna aina mbili kuu za mbolea ambazo ni:
1. Mbolea za asili (organic fertilizers)
2. Mbolea za viwandani (inorganic or industrial fertilizers)

Mbolea Za Asili (Organic Fertilizers)
Hizi ni mbolea zinazotokana na wanyama na mimea. Mbolea za asili ni kama vile: 
i.                    Mbolea vunde:
 inajulikana pia kama biwi au compost. Hutokana na mchanganyiko wa manyasi au mabaki ya mbao na samadi na majivu.
ii.                  Samadi:
 kutoka kinyesi cha wanyama kama mifugo na ndege.
iii.                Mbolea za kijani:
hutokana na kupanda mimea aina ya mikunde ambayo hukatuliwa na  kuchanganywa na udongo.
iv.                Majivu:
ni mbolea ya asili yenye madini aina ya potashi kwa wingi, fosfati, chokaa na magnesium.
v.                  Matandazo (mulch):
ambayo baadaye yakioza huwa mbolea.

Mbolea Za Viwandani (Inorganic Fertilizers)
Hizi ni mbolea zinazotengenezwa viwandani kwa kutumia virutubisho mbalimbali kwa kufuata viwango maalum vilivyowekwa ili kukidhi mahitaji ya mimea. Mbolea hizi zinatengenezwa kwa lengo maalum la kupata aina na kiasi fulani cha kirutubisho/ virutubisho vinavyohitajika na mimea.

Mbolea Za Kupandia
Mbolea maarufu za kupandia katika soko la Tanzania ni: TSP, DAP, Minjingu Phosphate na Minjingu Mazao. Lakini zile ambazo zimechaguliwa kwenye mradi wa ‘Kukuza matumizi ya Minjingu Phosphate’ ni DAP, Minjingu Phosphate na Minjingu Mazao.

                  1. Diammonium Phosphate (DAP)
Ina virutubisho viwili - naitrojeni ambacho kiko kwa kiwango cha asilimia 18, na fosfati (P2O5) ambacho kiko kwa kiwango cha asilimia 46. Inapatikana katika hali ya chengachenga (granules).

             2. Minjingu Phosphate
Ina kiwango cha fosfati (P2O5) asilimia 29 na inatumika zaidi kwa kutoa kirutubisho hiki. Lakini inaongeza vilevile kirutubisho cha chokaa (calcium) ambacho kipo kwa kiwango cha asilimia 40. Chokaa inasaidia vilevile kukabili tindikali (acidity) ya udongo.
                    
            3. Minjingu Mazao
Hii ni mbolea mpya inayotokana na Minjingu Phosphate lakini imeongezwa virutubisho vingine vitano ambavyo ni naitrojeni (10%), salfa (5%), zinki (0.5%), shaba (0.5%), boroni (0.1%), pamoja na chokaa (25% CaO) na magnesium (1.5% MgO). Virutubisho vilivyoongezwa hususani naitrojeni na salfa ni vile ambavyo vinakosekana katika aina nyingi za udongo.
Zinki, shaba na boroni vimeongezwa kwa tahadhari kwa sababu vinaonyesha dalili za upungufu katika baadhi ya maeneo. Minjingu Mazao iko katika hali ya chengachenga.

namna ya kuchagua mbolea ya kupandia
Mbolea za kupandia hasa Minjingu Phosphate na Minjingu Mazao zinahitaji hali maalum ya udongo ili ziweze kufanya kazi vizuri.
Kwa mfano hali ya tindikali ya udongo inabidi iwe chini ya 6.2 ili mbolea za Minjingu ziyeyuke kwa kiwango cha kutosha. Kwa udongo wenye tindikali zaidi ya 6.2, tumia DAP wakati wa kupanda. Ikiwa kuna upungufu wa potashi, tumia mbolea zinazorejesha madini hayo.

Tumia mboji pamoja na mbolea za viwandani ili kuongeza mazao. Mboji huwa haibebwi na mvua na faida yake hudumu kwa muda mrefu. Mboji husaidia udongo kuhifadhi maji na virutubisho. Zinapowekwa kwenye mashimo ya kupandia mbegu ni vyema kufukia mbolea kabla ya kuweka mbegu (kutenganisha mbolea na mbegu).

1. Upungufu Wa Naitrojeni (Nitrogen)
Kwa ujumla mmea unakuwa mdogo, mwembamba na hutoa suke dogo, na mwishowe hutoa mazao kidogo . Kama upungufu ni mkubwa sana mmea unaweza usitoe mazao. Kupungua kwa kasi ya ukuaji wa mmea - ambayo husababisha mmea kudumaa. Rangi ya kijani kwenye mmea hufifia na kugeuka taratibu kuelekea kwenye njano. Upungufu ukiwa mkubwa sana, majani hugeuka rangi ya njano kutoka pembeni. Majani yaliyokomaa ndio huanza kugeuka.Majani ya mwanzo hukauka mapema kwenye mimea yenye upungufu kuliko ile yenye naitrojeni ya kutosha.

2. Upungufu Wa Fosfati (Phosphorus)
Dalili ya kwanza ni kupungua kwa kasi ya kukua na mashina kuwa membamba. Upungufu ukiwa mkubwa, mmea unakuwa na rangi ya zambarau. Rangi hii inaanzia pembeni mwa majani na kwenye mashina na baadaye husambaa kwenye jani lote. Rangi inaonekana vizuri zaidi upande wa chini wa jani. Majani ya mwanzo hukauka mapema na mizizi haikui vizuri kwenye mimea yenye upungufu kuliko ile yenye fosfati ya kutosha.
 
3. Upungufu Wa Potashi (Potassium)
Kupungua kasi ya ukuaji wa mimea, ambayo inasababisha mmea kudumaa.
Upungufu ukiwa mkubwa rangi ya kijani inafifia na mwisho kutoweka kabisa na sehemu iliyoathirika inakauka (necrosis) kwenye mazao mengi , mazao mengine ya nafaka na miti ya matunda. Kutoweka kwa rangi ya kijani na kukauka kunaanzia pembeni mwa majani na kwenye
 ncha.}UYR$%Y#@ u nundu kama migongo ya bati (yellowish streaks and corrugated). Majani ya mwanzo hukauka mapema kwenye mimea yenye upungufu kuliko ile yenye potashi ya kutosha.

JINSI YA KUTUMIA MBOLEA WAKATI  WA  KUPANDA BILINGANYA
Mbolea hizi ni kama samadi, mbolea vunde na mbolea ya kuku.Weka kiasi cha tani 10 hadi 20 kwa hekta. Kiasi hiki ni sawa na kuweka ndoo moja hadi mbili zenye ujazo wa lita 20 katika eneo la mita mraba moja. Mbolea ya mchanganyiko aina ya N.P.K yenye uwiano wa 20:10:10 huwekwa kwenye shimo wakati wa kupandikiza mche. Kiasi kinachohitajika ni gramu tatu hadi tano (sawa na nusu kijiko mpaka kijiko kimoja kidogo cha chai) kwa kila shimo.
JINSI YA KUTUMIA MBOLEA WAKATI WA KUKUZIA BILINGANYA
Mbolea ya kukuzia aina ya CAN au S/A huwekwa wiki tatu baada ya mmea kuanza kutoa maua. Weka kiasi cha kizibo kimoja cha soda kuzungukia kila mche. Mbolea iwekwe katika umbali wa sentimita tano kutoka kwenye shina. Hakikisha mmea haugusi mche.
          Kukata kikonyo(kilele)
Wiki mbili baada ya kupandikiza miche, kata sehemu ya juu ya mmea (kilele) kama umepanda aina ndefu ya bilinganya. Hii itasaidia kupata matawi matatu hadi manne na mmea kutengeneza kupata matawi matatu hadi manne na mmmea kutengeneza umbile la kichaka. Matawi yakizidi manne yaondolewe ili kupata mazao mengi na bora.
     umwagiliaji wa bilinganya
Zao la bilinganya hustawi vizuri likipata maji ya kutosha kwasababu asili ya zao hili ni maji. Umwagiliaji ufanyike kila siku asubuhi na jioni kutegemea hali ya hewa ya sehemu husika.
KUVUNA
Bilinganya huanza kutoa matunda yaliyokomaa baada ya miezi miwili hadi mitatu tangu kupandikiza. Uvunaji huendelea kwa muda wa zaidi ya miezi minne na hauna budi ufanyike mapema mara tu matunda yanapokomaa. Matunda yaliyo komaa sana hayafai kuliwa kwa sababu huwa na kambakamba na mbegu zilizokomaa. Vuna mara mbili au tatu kwa wiki, kwa kutumia kisu kikali ili usiumize matunda.Kwa kawaida zao hili huzaa sana iwapo limetunzwa vizuri. Shamba lililotunzwa vizuri linaweza kutoa mavuno tani 50 hadi 60 kwa hekta. Hata hivyo mavuno mengi hutegemea aina ya bilinganya, umwagiliaji na rutuba ya udongo.
WADUDUWAHARIBIFU:
Ø  Vinyatomvu wa Bilinganya (Eggplant Lacebugs):
Wadudu hawa hushambulia zaidi sehemu ya chini ya jani. Hufyonza utomvu wa majani na kusababisha majani kuwa na mabaka meupe au njano.

 Mashambulizi yakizidi majani huanguka chini. Vinyatomvu wanaweza kuzuiwa kwa kunyunyizia moja ya dawa zifuatazo:-
Deltamethrin (Decis), Dimethoate (Sapa Dimethoate) Fenvalerate (Sumicidin), Lambda - Cyhalothrin (Karate).
Ø  Vidukari au Wadudu mafuta (Cotton Aphids):
Hawa ni wadudu wadogo wenye rangi nyeusi. Hushambulia majani machanga na kuyasababisha kudumaa na kukunjamana.

Zuia wadudu hawa kwa kutumia mojawapo ya dawa zifuatazo:- Dimecron 50% E.C, Lambda - Cyhalothrin (Karate) Dichlorvos (Nogos).
Ø  Utiriri wa Mimea (Red Spider Mites):
Ni vidudu vidogo vyenye rangi nyekundu iliyoiva. Hushambulia majani kwa kufyonza utomvu. Majani yaliyoshambuliwa huonyesha utando kama wa buibui.

Mashambulizi yakizidi mmea hudumaa, majani hukauka na hatimaye hufa. Utiriri unazuiwa kwa kutumia dawa zifuatazo:- Acrex, Karathane 25% W.P., Dimethoate, Ekalux, Kelthane.
Ø  Minyoo Fundo (Root knot nematodes):
Wadudu hawa hushambulia mizizi. Hutoa kinyesi ambacho ni sumukwammea. Sumu hii husababisba mizizi kuwa na nundu kama ya mizizi ya maharagwe.

Mashambalizi yakizidi mmea hudumaa, hunyauka na hatimaye hufa. Njia ya kuzuia wadudu hawa ni kubadilisha mazao. Kwa mfano; baada ya kuvuna zao hili, zao linalofuata lisiwe lajamii moja na bilinganya, kamavile nyanya, pilipili naviazi mviringo. Pia dawa aina ya Carbofuran (Furadan) inaweza kutumika.
MAGONJWA:
ü  Mnyauko Bakteria (Bacterial Wilt):
Ugonjwa huu husababishwa na backteria. Mmea ulioshambuliwa hunyauka ghafla hasa wakati wajua kali

Mnyauko bakteria unaweza kuzuiwa kwa kubadilisha mazao shambani. Endapo ardhi itashambuliwa na ugonjwa huu zao la bilinganya lisipandwe katika eneo hilo kwa muda wa miaka mitatu hadi mitano. Njia nyingine ni kupanda aina za bilinganya kama vile Matale, Kopek, na Rosita ambazo huvumilia mashambulizi ya ugonjwa huu.
ü  Phomopsis Vexans:

Ugonjwa huu husababishwa na bakteria na hushambulia majani, shina na matunda.

ü  Verticillium Wilt:
Huenezwa na maji na husababisha mmea kudumaa, majani kukunjamana na kuanguka.
Magonjwa ya Phomopsis Vexans na Verticillium Wilt yanaweza kuzuiwa kwa kung'oa na kuchoma moto mimea iliyoshambuliwa, kubadilisha mazao, na kuweka shamba katika hali ya usafi wakati wote.
Karibu sana shambani
MWISHO  WA MAKALA                                                                                                                                                                   Hemed Emmanuel Kangeta

 TEMBELEA  MAKALA  ZANGU  KWENYE MTANDAO  KANGETAKILIMO
·         Kilimo cha mihongo na mazao yote ya nafaka kama ufuta mbaazi ,choroko,mahindi ,karanga,nk
·         Kilimo cha vitunguu,pilipli,nyanya na mazao yote ya mbogamboga
·         Kilimo cha matunda kama mipesheni mipapai,michungwa,nk
·         Ufugaji wa kuku  wa kienyeji kisasa

Note
Makala hii hutotelewa bure bila ya malipo na atakae kuuzia wasiliana nami 

  (kangetakilimo) +255717274387:
Whatsapp no: +255717274387:
email: emmanuelkangeta@gmail.com
Instagram :kangetakilimo
facebook : kangetakilimo
WEB:KANGETAKILIMO
                           AU andika katika google search engine KANGETAKILIMO




No comments:

Post a Comment